VIONGOZI WAANDAMIZI WA TBN Wakutana Na Maafisa Wa Ubalozi Wa Marekani

 

Viongozi waandamizi wa Tanzania Bloggers Network (TBN) wakigonganisha glasi na Afisa Mahusiano ya Umma wa Ubalozi wa Marekani Bi. Marissa Maurer (wa tatu kushoto) na Afisa wa Siasa na Uchumi wa ubalozi huo Bw. Vincent Spera (wa pili kushoto) walipokutana jijini Dar es salaam kwa mazungumzo yasiyo rasmi ili kubadilishana mawazo ya njia bora ya kuendeleza tasnia hiyo ya habari za mtandao inayokuja juu kwa kasi nchini. 
TBN ni umoja wa bloggers wapatao 100 waliouunda ili kujiendeleza na kusimamia maslahi yao huku wakisaidia kusukuma mbele gurudumu la maendeleo ya Taifa nay a tasnia ya habari kwa jumla. Wengine toka kulia ni wajumbe wa TBN Max Mello, Joachim Mushi (Mwenyekiti), Monica Mara (Afisa Mipango), Hadija Kalili  (Katibu), Shamim Mwasha (mtunza hazina) na Afisa habari wa ubalozi huo Japhet Sanga. Picha kwa hisani ya TBN

Share this:

Post a Comment

 
Designed By TBN | Developed By Gadiola Emanuel