VIONGOZI WAANDAMIZI WA TBN Wakutana Na Maafisa Wa Ubalozi Wa Marekani

Friday, August 14, 2015

 

Viongozi waandamizi wa Tanzania Bloggers Network (TBN) wakigonganisha glasi na Afisa Mahusiano ya Umma wa Ubalozi wa Marekani Bi. Marissa Maurer (wa tatu kushoto) na Afisa wa Siasa na Uchumi wa ubalozi huo Bw. Vincent Spera (wa pili kushoto) walipokutana jijini Dar es salaam kwa mazungumzo yasiyo rasmi ili kubadilishana mawazo ya njia bora ya kuendeleza tasnia hiyo ya habari za mtandao inayokuja juu kwa kasi nchini. 
TBN ni umoja wa bloggers wapatao 100 waliouunda ili kujiendeleza na kusimamia maslahi yao huku wakisaidia kusukuma mbele gurudumu la maendeleo ya Taifa nay a tasnia ya habari kwa jumla. Wengine toka kulia ni wajumbe wa TBN Max Mello, Joachim Mushi (Mwenyekiti), Monica Mara (Afisa Mipango), Hadija Kalili  (Katibu), Shamim Mwasha (mtunza hazina) na Afisa habari wa ubalozi huo Japhet Sanga. Picha kwa hisani ya TBN

MNUSO WA TANZANIA BLOGGERS NETWORK (TBN) MEET AND GREET PARTY WAFANA SANA DAR ES SALAAM SERENA HOTEL JIJINI DAR

Sunday, March 01, 2015

 

Sehemu ya Wamiliki wa Blogs mbali mbali hapa nchini wakiwa kwenye picha ya pamoja na Mgeni Rasmi katika hafla maalum ya mwaka kwa Tanzania Bloggers Network,ambaye ni Katibu Mkuu wa Baraza la Habari Tanzania (MCT),Ndg. Kajubi Mukajanga pamoja na baadhi ya wadhamini waliofanikisha hafla hiyo,iliyofanyika usiku huu kwenye Hoteli ya Serena Jijini Dar es salaam.
Mgeni Rasmi katika hafla maalum ya mwaka kwa Tanzania Bloggers Network,Katibu Mkuu wa Baraza la Habari Tanzania (MCT),Ndg. Kajubi Mukajanga (wa pili kulia) akizungumza jambo na baadhi ya Wamiliki wa Blogs Tanzania,waliokutana pamoja leo kwa lengo la kufahamina na kuunganisha vyema umoja wao.

Mkurugenzi wa Masoko kwa Kampuni ya Simu ya Vodacom Tanzania ambao ndio walikuwa wadhamini wakuu,Kelvin Twissa akizungumza machache katika hafla hiyo. 

AU 
 
Designed By TBN | Developed By Gadiola Emanuel