Showing posts with label UCHAGUZI. Show all posts
Showing posts with label UCHAGUZI. Show all posts

TBN Yajumuika na Viongozi wa Habari Kuelekea Uchaguzi 2025

Sunday, August 24, 2025

 IMG-20250821-WA0058

Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Profesa Palamagamba Mwaluko Kabudi (wa nne kutoka kushoto waliokaa), akiwa kwenye picha ya pamoja na viongozi na wadau wa sekta ya habari na utangazaji baada ya kufungua Mkutano wa Wadau wa Habari na Utangazaji Kanda ya Mashariki uliofanyika jijini Dar es Salaam. Waliokaa kutoka kulia ni Meneja wa Huduma za Utangazaji wa Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA) Mhandisi Andrew Kisaka, Kaimu Mkurugenzi wa Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari Patrick Kipangula, Kaimu Mkurugenzi wa Idara ya Habari (MAELEZO) Rodney Mbuya, Katibu Mkuu wa Wizara ya Habari Gerson Msigwa, pamoja na Kamishna na Msemaji wa Jeshi la Polisi, DCP David Misime pamoja na Mjumbe wa Kamati ya Amani ya Mkoa wa Dar es Salaam. 

Waliosimama nyuma ni viongozi wa Mtandao wa Wanablogu Tanzania (TBN) akiwemo Muhidin Issa Michuzi (Mdhamini), Mwenyekiti wa TBN Beda Msimbe, Mjumbe Joachim Mushi na Mweka Hazina ambaye pia ni Mtaalamu wa Habari, Cathbert Kajuna.

IMG-20250821-WA0061
Dar es Salaam, Agosti 21, 2025: 

WAZIRI wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Profesa Paramagamba Kabudi, ametaja majukumu makuu matano ambayo sekta ya habari nchini inapaswa kuyatekeleza kuelekea Uchaguzi Mkuu wa Oktoba 2025, akisisitiza umuhimu wa taaluma, weledi na maadili katika kuripoti.

Akizungumza kwenye Mkutano wa Wadau wa Sekta ya Habari na Utangazaji Kanda ya Mashariki uliofanyika jijini Dar es Salaam, Profesa Kabudi alisema vyombo vya habari ni mhimili muhimu katika kukuza demokrasia na kulinda amani wakati wa uchaguzi.

“Vyombo vya habari vinapaswa kuhakikisha wananchi wanajua haki na wajibu wao, kutoa elimu juu ya sera za wagombea, kufuatilia ukiukwaji wa sheria za uchaguzi, kuhamasisha ushiriki wa makundi maalum kama vijana na wanawake, na kupambana na taarifa potofu badala ya kuzisambaza,” alisema Profesa Kabudi.

IMG-20250821-WA0057
IMG-20250821-WA0059

Aidha, alisisitiza kuwa utekelezaji wa majukumu hayo lazima uongozwe na misingi ya taaluma na maadili ya uandishi wa habari ili kulinda heshima ya tasnia na kuepusha vurugu au uvunjifu wa amani.

Kwa upande wake, Mkurugenzi wa Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari, Wakili Patrick Kipangula, alikumbusha waandishi wa habari kuhakikisha wanakuwa na ithibati kabla ya kufanya kazi za kihabari, hususan katika kuripoti uchaguzi.
IMG-20250821-WA0028
IMG-20250821-WA0031
IMG-20250821-WA0030

“Kifungu cha 19 cha Sheria ya Huduma za Habari kinasema bayana kuwa mtu yoyote anayetaka kufanya kazi ya uandishi ni lazima awe amepewa ithibati na Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari. Hivyo ni kosa la jinai kwa mwandishi wa habari kufanya kazi bila ithibati,” alisema Kipangula.

Aliongeza kuwa uhalali wa waandishi wa habari katika kipindi hiki ni jambo lisiloweza kupuuzia, kwani tasnia hiyo inahusisha majukumu makubwa yanayoathiri utulivu wa taifa.
IMG-20250821-WA0046(1)
Mkutano huo uliwahusisha wadau mbalimbali wa sekta ya habari na utangazaji, ambao walijadili nafasi ya vyombo vya habari katika kulinda maadili ya kitaifa na kuhakikisha wananchi wanapata taarifa sahihi kuelekea Uchaguzi Mkuu wa 2025.

Uchaguzi Mkuu 2025: INEC Yasisitiza Ushirikiano na Wazalishaji wa Maudhui Mtandaoni wakiwemo TBN

Tuesday, August 05, 2025



 

Mwenyekiti wa Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi (INEC), Mhe. Jaji wa Mahakama ya Rufani Jacobs Mwambegele akizungumza wakati wa ufunguzi wa mkutano wa Kitaifa wa Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi na Wazalishaji wa Maudhui Mtandaoni kuelekea Uchaguzi Mkuu wa Mwaka 2025. Mkutano huo umefanyika leo Agosti 3, 2025 Mlimani City Jijini Dar es Salaam.


MWENYEKITI Mwa Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi (INEC), Jaji wa Mahakama ya Rufani Jacobs Mwambegele ametoa wito kwa wazalishaji wa maudhui mtandaoni kuhakikisha taarifa zinazopandishwa katika kurasa zao zinakuwa za kweli na zisizo na chembe ya upotishaji ili kupeuka kuvuruga amani na utulivu wa nchi.

Jaji Mwambegele ametoa wito huo Agosti 3,2025 Jijini Dar es Salaam wakati akifungua mkutano wa kitaifa wa Tume huru ya taifa ya uchaguzi na wazalishaji maudhui mtandaoni kuelekea uchaguzi Mkuu wa mwaka 2025.

"Nawasisitiza na kuwakumbusha juu ya umuhimu wa kuepuka matumizi mabaya ya akili unde ambayo inatumiwa na baadhi ya watu wenye nia hovu kusambaza habari za upotoshaji hasa kupitia mitandao ya kijamii,"amesema.


Ameongeza kuwa tume hiyo ina matumaini makubwa na vyombo vya habari katika kufanikisha uchaguzi wa mwaka huu kupitia ushiriki wao.


"Imani hii inatokana na ushirikiano wenu mliouonesha tangu awali kwenye zoezi la uboreshaji wa daftari la kudumu la wapiga, mmekuwa wepesi wa kuwasilisha hoja na ushauri pale inapohitajika kila tunapokutana nanyi kwenye vikao,"ameongeza.

Awali akiwasilisha mada kuhusu maandalizi ya uchaguzi mkuu wa mwaka 2025 na ushiriki wa vyombo vya habari Mkurugenzi wa Uchaguzi Ramadhan Kailima amesema Tume inatarajia vyombo vya habari vitatumia kalamu zao na nyenzo walizonanzo kuhubiri amani katika kipindi chote cha mchakato wa uchaguzi.

"Tunawaomba na kuwasihi, kutumia nafasi na fursa mlizonazo kuhakikisha kunakuwepo na taarifa za mara kwa mara za kuelezea kinachoendelea kuhusu uchaguzi, "amesema.

Pia ameongeza kuwa vyombo vya ndivyo vinaweza kuwa sauti ya kwanza ya kuonesha upotoshwaji wa aina yoyote unaofanywa kwa bahati mbaya au makusudi kuhusu Tume na zoezi la uchaguzi Mkuu wa mwaka 2025.

"Tume imejiwekea utaratibu wa kuvishirikisha vyombo vya habari katika mchakato mzima wa uendeshaji wa uchaguzi huu ili kuweka uwazi na kuhakikisha wanashiriki kikamilifu, "ameongeza.

Mwenyekiti wa Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi (INEC), Mhe. Jaji wa Mahakama ya Rufani Jacobs Mwambegele akizungumza wakati wa ufunguzi wa mkutano wa Kitaifa wa Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi na Wazalishaji wa Maudhui Mtandaoni kuelekea Uchaguzi Mkuu wa Mwaka 2025. Mkutano huo umefanyika Agosti 3, 2025 Mlimani City Jijini Dar es Salaam.


Mwenyekiti wa Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi (INEC), Mhe. Jaji wa Mahakama ya Rufani Jacobs Mwambegele akizungumza wakati wa ufunguzi wa mkutano wa Kitaifa wa Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi na Wazalishaji wa Maudhui Mtandaoni kuelekea Uchaguzi Mkuu wa Mwaka 2025. Mkutano huo umefanyika Agosti 3, 2025 Mlimani City Jijini Dar es Salaam.
Mkurugenzi wa Uchaguzi wa Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi, Ndg. Kailima Ramadhani akiwasilisha mada wakati wa mkutano wa Kitaifa wa Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi na Wazalishaji wa Maudhui Mtandaoni kuelekea Uchaguzi Mkuu wa Mwaka 2025. Mkutano huo umefanyika Agosti 3, 2025 Mlimani City Jijini Dar es Salaam.
Mkurugenzi wa Uchaguzi wa Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi, Ndg. Kailima Ramadhani akiwasilisha mada wakati wa mkutano wa Kitaifa wa Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi na Wazalishaji wa Maudhui Mtandaoni kuelekea Uchaguzi Mkuu wa Mwaka 2025. Mkutano huo umefanyika Agosti 3, 2025 Mlimani City Jijini Dar es Salaam.

Mkurugenzi wa Uchaguzi wa Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi, Ndg. Kailima Ramadhani akiwasilisha mada wakati wa mkutano wa Kitaifa wa Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi na Wazalishaji wa Maudhui Mtandaoni kuelekea Uchaguzi Mkuu wa Mwaka 2025. Mkutano huo umefanyika Agosti 3, 2025 Mlimani City Jijini Dar es Salaam.

Baadhi ya wazalishaji Maudhui Mtandaoni wakiwa katika mkutano wa kitaifa wa Tume Huru wa Uchaguzi kuelekea Uchaguzi Mkuu wa Mwaka 2025. Mkutano huo umefanyika Agosti 3, 2025 Mlimani City Jijini Dar es Salaam.


Baadhi ya wazalishaji Maudhui Mtandaoni wakiwa katika mkutano wa kitaifa wa Tume Huru wa Uchaguzi kuelekea Uchaguzi Mkuu wa Mwaka 2025. Mkutano huo umefanyika Agosti 3, 2025 Mlimani City Jijini Dar es Salaam.


Baadhi ya wazalishaji Maudhui Mtandaoni wakiwa katika mkutano wa kitaifa wa Tume Huru wa Uchaguzi kuelekea Uchaguzi Mkuu wa Mwaka 2025. Mkutano huo umefanyika Agosti 3, 2025 Mlimani City Jijini Dar es Salaam.







Baadhi ya wazalishaji Maudhui Mtandaoni wakiwa katika mkutano wa kitaifa wa Tume Huru wa Uchaguzi kuelekea Uchaguzi Mkuu wa Mwaka 2025. Mkutano huo umefanyika Agosti 3, 2025 Mlimani City Jijini Dar es Salaam.








Baadhi ya wazalishaji Maudhui Mtandaoni wakiwa katika mkutano wa kitaifa wa Tume Huru wa Uchaguzi kuelekea Uchaguzi Mkuu wa Mwaka 2025. Mkutano huo umefanyika Agosti 3, 2025 Mlimani City Jijini Dar es Salaam.














Baadhi ya wazalishaji Maudhui Mtandaoni wakiwa katika mkutano wa kitaifa wa Tume Huru wa Uchaguzi kuelekea Uchaguzi Mkuu wa Mwaka 2025. Mkutano huo umefanyika Agosti 3, 2025 Mlimani City Jijini Dar es Salaam.


Baadhi ya wazalishaji Maudhui Mtandaoni wakiwa katika mkutano wa kitaifa wa Tume Huru wa Uchaguzi kuelekea Uchaguzi Mkuu wa Mwaka 2025. Mkutano huo umefanyika Agosti 3, 2025 Mlimani City Jijini Dar es Salaam.



Baadhi ya wazalishaji Maudhui Mtandaoni wakiwa katika mkutano wa kitaifa wa Tume Huru wa Uchaguzi kuelekea Uchaguzi Mkuu wa Mwaka 2025. Mkutano huo umefanyika Agosti 3, 2025 Mlimani City Jijini Dar es Salaam.





Baadhi ya wazalishaji Maudhui Mtandaoni wakiwa katika mkutano wa kitaifa wa Tume Huru wa Uchaguzi kuelekea Uchaguzi Mkuu wa Mwaka 2025. Mkutano huo umefanyika Agosti 3, 2025 Mlimani City Jijini Dar es Salaam.












Baadhi ya wazalishaji Maudhui Mtandaoni wakiwa katika mkutano wa kitaifa wa Tume Huru wa Uchaguzi kuelekea Uchaguzi Mkuu wa Mwaka 2025. Mkutano huo umefanyika Agosti 3, 2025 Mlimani City Jijini Dar es Salaam.


(PICHA ZOTE NA EMMANUEL MBATILO)
 
Designed By TBN | Developed By Gadiola Emanuel